Monday, September 28, 2015

DAWA YA MARADHI YOTE YA NGOZI YAPATIKANA

Kibaya Mwinyimbegu's photo.
MITEN OIL; DAWA YA MAGONJWA YA NGOZI. INATIBU:- FANGASI, UPELE, CHUNUSI, MAPUNYE, UTANGOTANGO, MAKUNYANZI, MUWASHO, KURAINISHA NGOZI N.K. INAPATIKANA KARIAKOO MTAA WA NYAMWEZI/MKUNGUNI KWENYE MADUKA YA DAWA ASILIA.



Mexime asema Simba iliponzwa na beki yake butu

NAHODHA wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Mecky Mexime Kianga amesema kwamba safu mbovu ya ulinzi iliwaponza Simba SC kufungwa mahasimu wao, Yanga SC Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba ilifungwa 2-0 na Yanga SC katika mchezo huo wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa mabao ya Amissi Tambwe kipindi cha kwanza na Malimi Busungu kipindi cha pili.

Akizungumza kwa simu kutoka Turiani, Morogoro, Mexime amesema kwamba Simba SC wanatakiwa kufanyia kazi safu yao ya ulinzi, vinginevyo itaendelea kuwagharimu. "Kilichowaumiza Simba ni kutokuwa na safu imara ya ulinzi," amesema.

Kuelekea mchezo wake na Yanga SC, Mexime amesema kwamba Mtibwa Sugar ina ukuta imara hivyo haitapa shida kwa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu.

"Mabeki wangu wako vizuri zaidi ukilinganisha na waliocheza juzi kwa upande wa Simba, yaani (alitaja jina la beki) ndio wanamtegemea, kwangu bado hajanivutia," aliongeza beki huyo na nahodha wa zamani wa Mtibwa Sugar na Taifa Stars.
Mtibwa Sugar wanatarajia kuikaribisha Yanga keshokutwa Jumatano katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara utakaofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.

Wakenya watawala mbio za Berlin Marathon


Image captionWakenya Eliud Kipchoge na Gladys Cherono ndio mabingwa wa mwaka huu wa mashindano ya Berlin Marathon yaliyofanyika leo huko Ujerumani.
Wakenya Eliud Kipchoge na Gladys Cherono ndio mabingwa wa mwaka huu wa mashindano ya Berlin Marathon yaliyofanyika leo huko Ujerumani.
Kipchoge ambaye pia ni bingwa wa mwaka huu wa mbio za london marathon alikuwa anazuru mji wa Berlin kwa mara ya pili.
Kipchoge aliandikisha ushindi wa saa mbili dakika na sekunde moja.
Katika mashindano yake ya kwanza huko Berlin Kipchoge alimaliz katika nafasi ya pili nyuma ya bingwa Wilson Kipsang aliyeandikisha muda bora wa saa 2 dakika 03 na sekunde 23.
Kufuatia ushindi wake Kipchoge anakuwa mwanariadha wa 15 kutoka Kenya kushinda mbio hizo.
Mkenya mwengine Dennis Kimetto aliandikisha rekodi ya dunia ya saa 2:02:57 mwaka wa 2014.

Kujitoa uhai:Vijana wengi wamo hatarini


Image captionVijana waliobalehe wamekuwa wakijiua kwa wingi katika mataifa yenye mapato ya chini
"Watu hudhani ni uhalifu kujiua, lakini sivyo hivyo, anasema Lauren Ball mwenye umri wa miaka 20 ambaye amejaribu kujiua kwa mara kadhaa.
Mara sita, huku jaribio lake la hivi karibuni likiwa lile la mwaka 2014.
''Najua imekuwa vigumu sana kwa familia yangu'," Ball alikiambia kipindi cha vijana cha BBC Newsbeat.
''Sidhani kama ni kitu ambacho naweza kukisahau, alisema mama huyo mwenye mtoto wa miaka 14 ambaye alijiua miaka miwili iliopita katika mji mmoja uliopo pwani ya mji wa Devon nchini Uingereza.
Jamii nyingi ndio zimeanza kuzungumzia kuhusu afya ya akili. Wengine bado hawazungumzii. Wakati huohuo wataalam wa masuala ya afya wameonya kuwa kuna umuhimu wa kukabiliana na janga la kujitoa uhai miongoni mwa vijana.
Suala ambalo limeonekana kama miko kwa muda mrefu,linasema shirika la afya duniani.

Sunday, September 27, 2015

TANZANIAN WEDDING2014 (ELIAS & MARTHA


NGASSA AANZA KUNG'ARA 'SAUZI'


MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mrisho Khalfan Ngassa alikuwa kivutio kikubwa leo wakati Free State Stars inaibuka na ushindi wa mabao 3-2 ugenini dhidi ya Maritzburg United katika Ligi Kuu ya ABSA Afrika Kusini.

Mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Harry Gwala, Ngassa alikuwa mpishi wa mabao yote matatu ya FS akicheza nafasi ya kiungo mchezeshaji.

Bao la kwanza lililofungwa na Danny Venter dakika ya 62 ilikuwa pasi ya Mrisho pamoja na la tatu lililofungwa na na Robert Sankara dakika ya 90.

Lakini Ngassa aliinua mashabiki Uwanja mzima wa Gwala baada ya kupiga chenga wachezaji wanne wa Meritsburg na alipofika kwenye boksi ili afunge mwenyewe, akaangushwa na kuwa penalti ambayo ilikwamishwa kimiani na Andrea Fileccia  dakika ya 80.

Mabao ya Meritburg yalifungwa na Kurt Lentjies kwa penalti dakika ya 65 na Mohammed Anas dakika ya 89. Mchezaji mwingine wa Tanzania, Uhuru Suleiman anayechezea Royal Eagles ya Daraja la Kwanza alikuwepo Uwanja wa Gwala kumtazama mwenzake akipiga kazi Ligi Kuu na baada ya mechi wakapiga picha ya pamoja.

Tuesday, November 4, 2014

Liverpool mdomoni mwa Madrid leo

Michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya inaingia mzunguko wa pili hii leo kwa mechi za marudiano ambapo mabingwa watetezi Real Madrid watakuwa nyumbani Santiago Bernabeu kukipiga na Liverpool..ambayo katika mechi ya awali ilikubali kichapo cha fedheha nyumbani Anfield.

MAKALA: TAARABU NI MUZIKI WA WASTAARABU, TAARABU SIO UGOMVI NA MABISHANO!!.

Na Kais Mussa Kais

MADADA WAKIAMULIWA UGOMVI.
Taarabu ni muziki wenye asili ya pwani, muziki huu hapo zamani ulikuwa ni maalum kwa ajili ya kuburudisha na kukufanya usahau machungu ya kutwa nzima kama ulikuwa shambani au ulikuwa katika kazi za ofisini. katka miaka ya 1960 taarabu ilishamili sana huko tanga na sehemu kadhaa wa kadhaa katika ukanda huu wa pwani ya mashariki.

  Mipasho katika taarabu haikuanza leo, ilikuwepo tangia enzi za wazee wetu, lakini mashairi waliyokuwa wanayatumia yalikuwa yanaficha maana hususani kwa asiejua maana! mtu anafumbiwa wala wa jirani yako hajui kama kuna mtu kasemwa, rusharoho ilikuwepo lakini sio ya kutiana vidole vya macho kama ilivyo kipindi hiki.

UNITED WANAKOSA UBORA- CARRICK

Michael Carrick

Nyota wa Manchester United, Michael Carrick, amekiri klabu hicho cha ligi ya Premier ya Uingereza kimekosa ubora unaohitajika kubobea kufikia sasa musimu huu lakini amepigia miamba hao upatu kuimarisha matokeo yao duni. 
 
Kufuatia kusalimu amri ugenini kwa maadui wao wa jadi, Machester City Jumapili, United wamezoa alama chache katika mechi 10 za kwanza za mwalimu wao mpya Louis Van Gaal kuliko zile walipata chini ya mtangulizi wake aliyefurushwa, David Moyes.

United wamejipata alama 13 nyuma ya vingozi Chelsea na alama sawa na pengo hilo lakini Carrick amesisitiza United wako kwenye mkondo wa kutamba tena hivi karibuni.

“Tukiangalia jumla ya alama zetu, tunajuta pakubwa kwani hatuko katika kiwango kinachohitajika. Lakini ukichunguza kwa makini, kuna dalili tutakuwa na musimu mwema.

AZAM FC NAKO KWAWAKA MOTO.

Kufuatia kupata vipigo viwili mfululizo toka kwa JKT Ruvu ya Pwani 1-0 na Ndanda FC ya Mtwara 1-0 hali si shwari ndani ya klabu ya Azam FC baada ya kocha wake msaidizi Kalimangonga Ongalla kubwaga manyanga.

Taarifa za ndani toka Azam zinasema Ongalla ameamua kujiuzulu nafasi yake hiyo na ataondoka nchini kuelekea Uingereza kujiendeleza na taaluma yake ya ukocha.

Lakini mtandao huu umebaini kuwa vipigo viwili mfululizo ndio vimepelekea kocha huyo kubwaga manyanga.

Azam imekuwa na wakati mgumu ktk mechi zake za karibuni, mabingwa hao wa bara 2013/14 wamejikuta wakitibua rekodi yao ya kucheza mechi 38 bila kupoteza.

Azam inayonolewa na Mcameroon Joseph Omog imekubali vipigo toka kwa JKT Ruvu cha bao 1-0 ktk uwanja wake wa Chamazi, pia ikakubaki kipigo kingine cha ugenhni toka kwa Ndanda FC 1-0 ktk uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

ETI YANGA INA MCHEZAJI MMOJA TU ANAYECHEZA KIKOSI CHA KWANZA

KOCHA wa Kagera Sugar, Jackson Mayanja amesema kuwa kiungo Mbrazil wa Yanga Andrey Coutinho ndiye mchezaji pekee anayeibeba Yanga kwa sasa lakini akadai hiyo kwa sasa inacheza kama imechoka tofauti na msimu uliopita.

Mayanja, raia wa Uganda alisema; “Yanga wana kiungo mmoja mzuri ambaye ni Coutinho, anajua kucheza kwa kasi na ana akili nzuri ya soka. Huyo ndiye mchezaji anayeweza kuisaidia Yanga kwani kwa staili wanayocheza Yanga kwasasa ni ile isiyoweza kuwapa ushindi kirahisi.”

“Yanga kwa msimu huu imepoteza kasi tofauti na msimu uliopita na ili warudishe kasi hiyo lazima benchi la ufundi lifanye kazi ya ziada,” alisema kocha huyo ambaye timu yake iliichapa Yanga bao 1-0 Jumamosi iliyopita japokuwa alikuwa jukwaani akitumikia adhabu ya kadi nyekundu.

Katika hatua nyingine kocha huyo ametamka wazi kuwa Yanga haikuwa na sababu ya kumsajili Mbrazil Geilson Santos ‘Jaja’ na badala yake wangetulia na wachezaji wazawa wenye uwezo mkubwa.

Monday, November 3, 2014

Phiri:Sare Simba siri nzito

Wakati Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri, akisema matokeo ya sare ambayo timu yake imeendelea kuyapata katika mechi za Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara yana siri nzito na yanazidi kumchanganya, Mecky Maxime anayeinoa Mtibwa Sugar amekivulia kofia kikosi cha Mzambia huyo kwa kusema kinakosa bahati tu.

Simba juzi iliendelea kupata sare na kufikisha pointi sita katika mechi sita walizocheza katika Ligi ya Bara msimu huu ambayo ilianza kupigwa kwenye viwanja mbalimbali nchini tangu Septemba 20, mwaka huu.

Sare ya juzi ya bao 1-1 dhidi ya Mtibwa Sugar waliyoipata Simba kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani hapa, imeifanya timu hiyo kuendelea kusuasua msimu huu huku ikiwa benchi la ufundi likiwa limepewa mechi mbili za kusaka matokeo mazuri.

Villa wateleza na kulazwa na Spurs

Harry Kane

Aston Villa walifunga bao lao la kwanza baada ya kukaa zaidi ya saa tisa bila bao lakini mambo yakawaendea mrama Christian Benteke alipofukuzwa uwanjani na Tottenham Hotspur wakajikwamua na kushinda 2-1 mechi iliyochezewa Villa Park Jumapili.

Hilo kilikuwa kichapo cha sita mfululizo Ligi ya Premia, licha ya Andreas Weimann kumaliza ukame wa mabao kwa kufunga krosi ya Charles N'Zogbia dakika ya 16.

Lakini straika wa Ubelgiji Benteke alifukuzwa uwanjani dakika ya 20 baada ya kipindi cha pili kuanza kwa kumgonga Ryan Mason usoni kwa kutumia mkono wake baada ya mtafaruku uliohusisha wachezaji kadha.

MILOVAN CIRKOVIC KUMRITHI PHIRI SIMBA

Wakati siku za kocha mkuu wa Simba Mzambia Patrick Phiri zinahesabika, uvumi umeenea kuwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo Mserbia Milovan Cirkovic yuko mbioni kurejea Simba.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari ambacho kipo karibu na mabosi wa klabu hiyo kinasema kuwa Milovan ni chaguo la kwanza endapo ataondoka Phiri.

Milovan ni kocha mzuri aliyewahi kuibebesha ubingwa Simba mara kadhaa kilisema chanzo hicho. Aidha mabosi hao wamewaambia wanachama na mashabiki wa Simba wajiandae kupata furaha mara baada ya kuwasili kocha huyo.

Milovan atakumbukwa sana na mashabiki wa Simba hasa baada ya kuipa kipigo cha kihistoria Yanga cha mabao 5-0 ambacho hadi leo hakijasahaulika.

Wednesday, October 15, 2014

MMILIKI WA FACEBOOK AMENUNUA HUU UPANDE WA KISIWA CHA HAWAII

Hekari hizo 700 zitajumuisha beach resort, mashamba ya miwa na kilimo hai ambapo kwa sheria za Hawaii beach resort hiyo lazima iachwe wazi kwa matumizi ya jamii kwa sababu kisiwa hiko hakina sheria ya umiliki binafsi wa mchanga.